Loading...

BREAKING NEWS: GODBLESS LEMA KIBOKO AFANYA TUKIO LA AJABU NA KUACHIWA

Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema amepandishwa mahakamani katika kesi mbili tofauti.

Kesi ya kwanza namba 351/2016 anatuhumiwa kumtumia ujumbe wa simu wa uchochezi Mkuu wa mkoa Arusha, Mrisho Gambo wenye maneno kuwa “Karibu tutakudhibiti kama mashoga walivyodhibitiwa Uarabuni”

Kesi ya pili namba 352/16 Lema anatuhumiwa kuhamasisha maandamano Septemba Mosi kinyume cha sheria.

Hakimu amepinga hoja za wakili wa Serikali,  Vincent Njau kuzuia dhamana kwa sababu za kiinterejensia kwa usalama wake.

Lema amekana mashitaka yote, na ameachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ambapo kwa shitaka la kwanza alitakiwa kupata mdhamini na shilingi 10, na shitaka la pili dhama ni shilingi milioni 15.Kesi hiyo itatajwa tena Septemba

Hakimu anayesikiliza kesi ni Desderi Kamugisha wakati wakili wa serikali akiwa ni Innocent Njau.

Baadaye vurugu ziliibuka mahakamani wakati polisi wanataka kumpeleka Lema magereza kwa madai kuwa wadhamini wamechelewa, lakini mbunge huyo alipinga hatua hiyo kwa maelezo muda wa mahakama saa 9.30 ulikuwa bado.

STOP Stage Managing Violence, I DID NOT GATECRASH Dandora Rally- Sonko Tells CS Eugene Wamalwa, Wanjiru

Nairobi senator Mike Sonko Mbuvi has refuted reports that he gatecrashed CS Eugene Wamalwa and Bishop Margret Wanjiru meeting in Dandora on Saturday. The senator confirmed that he was officially invited and even at the rally his seat was reserved.

They are stage managing the events to show that I am violent. I was officially invited and my seat was reserved for me. Kina eugine were just scared the way my supporters were cheering me and escorting me to the dais
Meanwhile as most Nairobian are struggling to get access to clean water both Nairobi governor Evans Kidero and Water CS Eugene Wamalwa are not offering any solutions despite the fact that both have mandate to serve the residents.
CS Wamalwa is in charge of Water and irrigation, he should strive to make sure Nairobians have clean water in abundance now that he wants to be governor, he should demonstrate his prowess in service delivery instead of dogging Margret Wanjiru
While CS Eugene is clearly contraving the constitution by engaging in politics while in office as CS, senator Sonko is giving temporary solutions to the current water crisis being experienced in the city. Today his team supplied over 100,000 litres of water to the residents of mathare, huruma and mlango kubwa

BREAKING: Uhuru SUCCUMBS to PRESSURE from Raila Led Mwanainch to ASSENT to the INTEREST RATES BILL, Big Win for Kenyans

President Uhuru Kenyatta has finally assented to the Banking Amendment Act 2015 as passed by parliament in July.BREAKING: Uhuru SUCCUMBS to PRESSURE from Raila Led Mwanainch to ASSENT to the INTEREST RATES BILL, Big Win for Kenyans
The law will cap commercial interest rates at 400 basis points above the central bank’s benchmark rate, which currently stands at 10.5 per cent.
At the current rate a borrower will get a loan at 14.5 per cent, (CBR 10.5+4 (Proposed cap). Prime Minister Raila Odinga led Kenyans in pilling pressure on the president to sign the bill. Uhuru family has fast interests in banking sector.
HERE is President Uhuru’s Statement
On July 28, 2016, the National Assembly passed the Banking (Amendment) Bill, 2015. The Bill intends to regulate interest rates that are applicable to banks’ loans and deposits, capping the interest rates that banks can charge on loans and must pay on deposits.
In line with the Constitution of Kenya the Bill was presented to me, for appropriate action as required by law.
Since receiving this Bill, I have consulted widely and it is clear to me from those consultations that Kenyans are disappointed and frustrated with the lack of sensitivity by the financial sector, particularly banks. These frustrations are centred around the cost of credit and the applicable interest rates on their hard–earned deposits. I share these concerns.
This is the third time that the National Assembly is attempting to reduce interest rates to affordable levels. In the previous two instances, dialogue and promises of change prevailed and banks avoided the introduction of these caps. In those instances, banks failed to live up to their promises and interest rates have continued to increase along with the spreads between the deposit and lending rates.
Despite having one of the most efficient and effective financial markets, Kenya has one of the highest returns-on-equity for banks in the African continent. Banks need to do more to reduce the cost of credit and ensure that the benefits of the vibrant financial sector are also felt by their customers.
Upon weighing carefully all these considerations, on balance, I have assented to the Bill as presented to me. We will implement the new law, noting the difficulties that it would present, which include credit becoming unavailable to some consumers and the possible emergence of unregulated informal and exploitative lending mechanisms.
We will closely monitor these difficulties, particularly as they relate to the most vulnerable segments of our population. Whilst doing so, my Government will also accelerate other reform measures necessary to reduce the cost of credit and thereby create the opportunities that will move our economy to greater prosperity.
We recognize that banks have done much in the last decade in terms of innovation and promoting financial inclusion and look to their doing more in that direction.
We also reiterate our commitment to free market policies in driving sustainable economic growth, to which we owe much of our success.
Uhuru Kenyatta, CGH
President of the Republic of Kenya
Wednesday 24th August 2016

Breaking News: Tundu Lissu aibuka tena na sakata jipya na Mkuu wa Upelelezi kanda Maalum Dar es Salaam (zco)

 Camilius Wambura, Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalum ya Dar es Salaam (ZCO) (picha kubwa). Picha ndogo ni Tundu Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chadema
CAMILIUS Wambura, Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalum ya Dar es Salaam (ZCO), ametakiwa kufika mahakamani kama shahidi katika kesi ya uchochezi inayomkabili Tundu Lissu, Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, anaandika Faki Sosi.
Maombi ya kumtaka Wambura kufika mahakamni hapo, yametolewa na Peter Kibatala, wakili wa upande wa utetezi katika kesi hiyo ambayo Lissu anatuhumiwa kutoa maneno ya uchochezi kwa kumuita Rais John Magufuli kuwa ni ‘dikteta Uchwara’.
Lissu anadaiwa kutamka maneno hayo mara baada ya kutoka mahakamani katika kesi nyingine inayomkabili ya kutoa maneno ya uchochezi kupitia gazeti la MAWIO.
Kibatala amedai kuwa, kabla ya mashahidi wengine kutoa ushahidi, ni vyema mahakama imuite Mkuu wa Upelezi Kanda Maalum ya Dar es Salaam ili afike mahakamani hapo, kutoka maelezo kama sehemu muhimu ya kesi kutokana na yeye kuwa ndiye mtoa taarifa.
“Tunaiomba Mahakama iwaamuru upande wa mlalamikaji kumleta ZCO kutokana na ukweli kuwa, maelezo yake ni sehemu ya ushahidi hasa katika mashitaka haya yanayohusu sheria ya magazeti. Maelezo yake ni muhimu ili mshitakuwa aweze kujitetea,” amedai Kibatala.
Bernad Kongola, Wakili wa serikali akijibu hoja za Kibatala amedai kuwa, mkuu wa upelelezi sio shahidi katika kesi hiyo hivyo hakuna sababu ya kuitwa mahakamani hapo.
Kongola amesema, upande wa serikali tayari unao mashahidi na kuwataja kwa majina kuwa ni ASP Kimweri, na Sub-Sajenti. Ndege. Yohona Yongola, Hakimu Mkazi Mahakama ya Kisutu, amesema kuwa uamuzi wa hoja zilizotolewa na pande mbili juu ya kuletwa kwa mkuu wa upelelezi kanda maalumu ya Dar, ataufanya tarehe 6 Septemba mwaka huu.

Breaking News: KIMENUKA TENA KWA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA NCHINI, SIKU 2 TU ZATOLEWA

MSAJILI wa Vyama Siasa, Jaji Francis Mutungi, ameitisha mkutano maalum wa baraza la vyama hivyo utakaofanyika jijini Dar es Salaam Jumatatu na Jumanne ijayo, kujadili hali ya siasa iliyopo nchini kwa sasa.
 Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Jaji Mutungi alisema baraza litajadili sintofahamu inayoendelea katika duru za siasa.
Jaji Mutungi alisema katika mkutano huo wanatarajia kualika watu ambao wanaamini watasaidia kufanikisha mazungumzo hayo.
Kwa habari zaidi nunua nakala ya NIPASHE LEO

BREAKING NEWS: VIJANA WA KAZI WAFANYA KWELI...HAYA NDIO WALIOKUWA WANAYATAFUTA BAVICHA

 Picha kubwa ni Jeshi la polisi wakipambana na wafuasi wa Chadema, Salum Mwalimu, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema – Zanzibar (Picha ndogo ya kwanza)
BARAZA la Vijana Taifa la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bavicha), limesema Jeshi la Polisi linawajibu wa kikatiba wa kulinda operesheni yao ya Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania (Ukuta),anaandika Faki Sosi.
Pastrobas Katambi, Mwenyekiti wa Bavicha, akizungumza na waandishi wa habari leo Makao Makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam, amesema vyama vya siasa vipo kwa mujibu wa katiba na kwamba vinahaki ya kupatiwa ulinzi vinapofanya mikutano ya hadhara na maandamano.
Katambi amesema jeshi hilo litakuwa linatimiza jukumu lake la kikatiba likishirikiana na Chadema kufanikisha maandamano yaliyopangwa kufanyika nchi nzima Septemba mosi.
Amesema ni upotoshaji mkubwa wa hali halisi pale jeshi la polisi linaposhiriki kampeni ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inayolenga kuyadhibiti maandamano hayo.
Amesema wapo viongozi wa CCM wenye nia mbaya ambao wanaeneza kampeni kwamba maandamano hayo ni ya uchochezi.
“Sio kweli kuwa Ukuta ni uchochezi na wanaosema hivyo wanalenga kupitisha ajenda yao ya kukichafua chama pamoja na kupandikiza chuki kwa wananchi dhidi ya Chadema,” amesema.
Katambi amesema wakuu wa wilaya na mikoa na wenyewe wanajukumu la kusimamia sheria na katiba ya nchi badala ya kuchukua mkondo wa kutaka kukandamiza demokrasia.
Amesema ni udhaifu tu wa mamlaka ya uteuzi wa viongozi serikalini kuteua makada wa CCM kuwa ndio wanaoshika nyadhifa hizo ambazo huwafanya moja kwa moja kuwa wenyeviti wa Kamati za Ulinzi na Usalama kwenye maeneo yao. Hiyo huwasukuma kutumikia wananchi kwa utashi wa kisiasa kuliko kuzingatia sheria.
Katambi amesema Bavicha limejipanga kuwalinda viongozi wa chama ili wasije kukamatwa kama inavyosemekana polisi kuazimia kufanya hivyo kabla ya siku ya maandamano.
Katika hatua nyingine, Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) umetangaza kuandaa maandamano nchi nzima tarehe 31 mwezi huu.
Shaka Hamdu Shaka, Katibu wa umoja huo amewaambia waandishi wa habari leo kwamba maandamano hayo ni ya kumpongeza Rais John Magufuli kwa alichosema “hatua anazochukua Rais huyo katika kuinua uchumi.”
Shaka amesema wamemuandikia barua Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) Ernest Mangu kutaka ruhusa ya kufanya maandamano hayo aliyosema ni ya amani.
Msemaji wa jeshi hilo hakupatikana kuthibitisha kama wamepokea barua hiyo.

Lipumba Aipasua CUF, Wajumbe Warushiana Viti na Kutukanana, Mkutano Wavunjika

Mkutano Mkuu Maalum wa Chama Cha Wananchi (CUF), uliofanyika jana jijini Dar es Salaam ukilenga kuwachagua Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho ulivunjika baada ya wajumbe kuanza kurushiana viti na matusi baada ya kupishana katika hoja ya kumtosa aliyekuwa Mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba.

Profesa Lipumba alijiuzulu nafasi yake kabla ya kampeni za uchaguzi Mkuu mwaka jana akieleza kuwa roho inamsuta kumnadi mgombea urais aliyeungwa mkono na vyama vya Ukawa. Lakini mwaka huu alirejea na kuandika barua akiomba kurejea kwenye nafasi yake hali iliyozua sintofahamu.

Taarifa kutoka ndani ya Mkutano huo zimeeleza kuwa wajumbe 832 walihudhuria lakini hoja ya kumjadili Profesa Lipumba ilipofikiwa, baadhi ya wajumbe ambao wanamuunga Mwenyekiti huyo wa zamani walizua vurugu wakipinga utaratibu uliotumika.

Baadhi ya wajumbe hao waliwaambia waandishi wa habari kuwa viongozi waliopo madarakani walifanya ubabe kwa kulazimisha kura ya kukubali au kukataa ombi la Lipumba ipigwe kwa uwazi na sio siri kama Katiba inavyoeleza.

“Haki haikutendeka, ni ubabe. Wala mkutano haikuzingatia kutimia kwa akidi. Tulilazimishwa kupiga kura kwa kunyoosha mikono wakati mazingira yaliyopo na usahihi, kura ni siri,” mmoja wa wajumbe hao alikaririwa.

Baada ya kupiga kura za wazi, Lipumba alipata kura 14 kati ya kura 832 hivyo kuonekana kukataliwa kwa kishindo, lakini vurugu zilizuka ghafla kutokana na maamuzi hayo na mkutano ukashindwa kufanikisha zoezi zima la kuwapata viongozi hao wapya.

Katika hatua nyingine, Juma Haji Duni alijiengeu katika kinyang’anyiro cha uchaguzi huo, baada ya baadhi ya wajumbe kusisitiza kuwa katiba inamtaka mtu aliyejiuzulu na kuhamia chama kingine kusubiri miaka miwili ili agombee nafasi ya uongozi ndani ya chama pale atakaporejea.

Mkurugenzi wa Uchaguzi na Mipango wa CUF, Shaweji Mketo, alisema kuwa Duni alijiondoa kutokana na maadui wa Ukawa kutaka kukihujumu chama hicho.

Mkutano huo umeahirishwa hadi utakapotangazwa tena.

TUNDU LISSU AFANYA YAKE TENA KWA MARA NYINGINE TENA KWA MAAJABU YA HALI YA JUU

Serikali imeendelea kupigwa mweleka katika kesi ya uchochezi dhidi ya mshitakiwa Tundu Lissu baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kutupa pingamizi la Wakili wa Serikali wakitaka wakili Peter Kibatala kujitoa kumtetea mwanasiasa huyo.

Lissu, ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki kwa tiketi ya Chadema alipandishwa kizimbani Agosti 5, na kusomewa mashtaka matatu, mawili kati yake yakiwa ni ya uchochezi na moja la kuidharau mahakama.

Pigo la kwanza la upande wa mashtaka ni pale Lissu alipopangua hoja na kufanikiwa kupata dhamana, wakati kesi hiyo ilipofikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza.

Jana ilikuwa ushindi mwingine kwa upande wa utetezi, baada ya Mahakama kutupa pingamizi la upande wa mashtaka lililotaka Kibatala ajitoe katika jopo la mawakili wanaomtetea Lissu.

Upande wa mashtaka ulioongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Faraja Nchimbi, uliweka pingamizi hilo kwa maelezo Kibatala ni shahidi wao kwa kuwa alikuwapo siku na mahali wakati Lissu akitoa maneno yanayodaiwa ya uchochezi.

Wakili Kibatala ambaye ni kiongozi wa jopo la mawakili wanaomtetea Lissu, alipinga hoja za Serikali za kutaka ajitoe katika kesi hiyo, mvutano ambao ulisababisha kesi hiyo kuahirishwa mara mbili.

Wakili Kibatala alipinga kuwa hakuna kifungu cha sheria kinachomzuia wakili kumtetea mteja wake kwa sababu tu ya kushuhudia akitoa maelezo yake Polisi.

Akitoa uamuzi wa pingamizi hilo la Serikali, Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha anayesikiliza kesi hiyo, hakukubaliana na hoja za upande wa Jamhuri (mashtaka) na hivyo akalitupa pingamizi hilo.

Hakimu Mkeha alikubaliana na hoja za wakili Kibatala kuwa hakuna kifungu chochote cha sheria kinachomzuia kumtetea Lissu.

Alisisitiza kuwa Kibatala ataendelea kuwa wakili wa Lissu katika kesi hiyo na kwamba kama upande wa mashtaka ukimhitaji awe shahidi wao utalazimika kumuomba. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 19.

Breaking News: JANA MAHAKAMANI KISUTU PALIKUWA PAZITO NA HAYA NDIO MAAMUZI YALIYOTOLEWA KWA LISSU, HAKIMU "MFAWIDHI" NI KIBOKO

 Wakili Peter Kibatala
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imetoa uamuzi wa hoja zilizokuwa zikibishaniwa na mawakili wa pande mbili katika kesi ya uchochezi inayomkabili Tundu Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), anaandika Faki Sosi.
Hoja zilizotolewa na upande wa mashtaka wakati kesi hiyo ilipotajwa kwa mara ya kwanza, ya kwamba wakili Peter Kibatala hana uhalali wa kumtetea Lissu katika kesi hiyo kutokana na kuwa ni mmoja wa mashahidi wa upande wa Jamuhuri, ilikuwa ikitolewa uamuzi.
Cyprian Mkeha, Hakimu Mfawidhi katika mahakama hiyo ametoa uamuzi wa shauri hilo kwa kutupilia mbali hoja za upande wa mashitaka.
Hakimu Mkeha, amesema kuwa, hakuna sheria yoyote inayomzuia Kibatala kumtetea mteja wake kama upande wa mashitaka ulivyodai na hivyo ataendelea kumtetea Lissu.
Baada ya uamuzi huo kutolewa, kesi hiyo itatajwa tena tarehe 19 Septemba mwaka huu.

Breaking News: Rais Magufuli Kiboko ‘awakomoa’ Chadema Arusha

 Mrisho Gambo, Mkuu wa Mkoa wa Arusha
RAIS John Magufuli amemteua Mrisho Gambo aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha (Mjini) kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha na kumng’oa Felix Kijiko Ntibenda aliyekuwa akishikilia wadhifa huo,anaandika Charles William.
Gambo ambaye kwa muda wa mwezi mmoja sasa, amekuwa katika mgogoro na Godbless Lema, Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini kutokana na kile kinachotajwa kuwa ni kuingiliana majukumu, amepandishwa wadhifa katika mazingira yanayoaminika kuwa, ni ya kimkakati zaidi.
Mwanzoni mwa mwezi huu, Lema na Gambo walishambuliana vikali mbele ya Seleman Jafo, Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), katika kikao cha pamoja cha watendaji wa Halmashauri ya Jiji la Arusha.
Katika kikao hicho, Lema alisema Gambo amekuwa akiingilia uamuzi unaopitishwa na Baraza la Madiwani la halmashauri hiyo lenye diwani mmoja tu wa CCM kati ya 33.
Huku akitoa mfano kuwa, Kamati ya Mipango Miji ilikuwa imeandaa ziara ya kikazi lakini katika hali ya kushangaza, Gambo alimwagiza Athuman Kihamia, Mkurugenzi wa Jiji la Arusha aisitishe.
Hata hivyo, Gambo akijibu tuhuma hizo alisema, yeye ndiye rais wa wilaya hiyo kwa sababu anafanya kazi kwa niaba ya Rais Magufuli.
“Mbunge atambue huduma za wananchi hazisubiri maamuzi ya Baraza la Madiwani kwani, haiwezekani kila kamati kutembelea mradi mmoja wa elimu, afya au miradi mingine, Mimi ndiye rais wa wilaya na ninafanya kazi bila kukurupuka,” alisema Gambo.
Katika mvutano huo baina ya Lema na Gambo, Naibu Waziri Jafo alimwagiza Richard Kwitega, Katibu Tawala Mkoa wa Arusha, kutatua mgogoro huo na kuhakikisha kila kiongozi anafanya majukumu yake, pasipo mwingiliano.
Hata hivyo, wawili hao wameendelea kurushiana maneno katika siku za hivi karibuni, Lema amenukuliwa akisema, “Gambo ameingia Arusha na kiherehere huku akikurupuka na kuingilia majukumu yasiyomuhusu.”
Huku Gambo naye akinukuliwa akisema, “Mimi ni mzoefu wa kazi ya ukuu wa wilaya kwa zaidi ya miaka mitano sasa, sihitaji kufundishwa majukumu yangu na mbunge.”
Kupandishwa wadhifa kwa Gambo, kunaashiria kuwa, Ikulu chini ya Rais Magufuli imefurahishwa na kazi yake. Kunaashiria pia katika mgogoro uliokuwa ukiendelea Arusha, Gambo alikuwa akifanya kazi inayokubalika na yenye baraka za Ikulu.
Richard Kwitega, Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha ambaye aliagizwa na Jafo kutatua mgogoro wa Gambo na Lema, sasa atakuwa chini ya Gambo. Atakuwa msaidizi wa Mkuu huyo mpya wa Mkoa na atakuwa akifanya kazi kwa maelekezo ya ‘bosi’ huyo.
Itakumbukwa kuwa, katika matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana, Chadema ilishinda ubunge katika majimbo sita huku CCM ikiambulia jimbo moja tu katika Mkoa wa Arusha na katika Halmashauri ya Jiji hilo, Chadema ilishinda udiwani katika kata 24 na CCM ikiambulia kata moja.
Naam, unaweza kuelezea kitendo cha Gambo kupandishwa wadhifa na Rais Magufuli kwa maneno mengi na kwa namna tofauti tofauti lakini ukisema, “Rais Magufuli amewakomoa Chadema Arusha,” hutakuwa mbali na ukweli.

Breaking News: Madudu Dodoma

Majaliwa Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWAKATI serikali ikijiandaa kuhamia Mkoa wa Dodoma, Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali za Mitaa imebaini kuwepo kwa madudu katika Sekretarieti ya mkoa huo, anaandika Dany Tibason.
Kamati hiyo imebaini kuwepo kwa matumizi mabaya ya fedha za serikali ikiwa ni pamoja na kujiuzia magari ya serikali bila kufuata utaratibu. 
Japhet Hasunga, Mwenyekiti wa Kikao cha Kamati ya PAC ambaye ni Mbunge wa Vwawa (CCM) amesema, watumishi wamekuwa wakijiuzia magari ya serikali, wakipeana pia wakiyatengeneza katika gereji bubu.
Mbali na hayo pia kuna sintofahamu kuhusu ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma ambao kamati hiyo imehoji sababu ya kununuliwa kwa vifaa vipya wakati jengo halijakamilika.
Kutokana na kuwepo kwa madudu hayo katika Sekretalieti ya Mkoa wa Dodoma, PAC imetoa maagizo saba kwa uongozi wa mkoa kutokana na kushindwa kujibu hoja kutokana na Ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG).
Hasunga ameagiza mambo saba; kwanza, kamati imeitaka idara ya usimamizi wa mali za serikali kufanya uhakiki maalum wa mali za serikali katika fungu 72 hasa magari yanayofanya kazi, yaliyoharibika na yaliyouzwa na kuwasilisha taarifa ya uhakiki huo maalumu kwa kamati ndani ya miezi mitatu.
Amemtaka Ofisa Masuhuri kusimamia kitengo cha uhasibu ili kuzingatia viwango vya kimataifa ya utayarishaji wa mahesabu katika utayarishaji wa mahesabu ya serikali ili kuepuka hati za ukaguzi zenye dosari.
Akitoa maagizo amesema, kamati inamwagiza Ofisa Masuhuri kuzingatia sheria ya manunuzi ya mali ya umma na kanuni zake katika shughuli za sekretalieti ikiwa ni pamoja na kupata vibari kwenye mamlaka husika anapofanyika uhamisho wa fedha katika vifungu mbalimbali.
Mbali na hilo kamati imemuomba CAG kwa kushirikiana idara ya mali za serikali kufanya tathimini ya kina kuiridhisha kamati iwapo garama za Sh. 12.5 Mil zilizotumika katika ujenzi wa jengo la ofisi ya mkuu wa mkoa kama zinakidhi thamani halisi ya sasa.
Hasunga pia ametoa agizo la tano kuwa Ofisa Masuhuri awasilishe taarifa ya maandishi kuhusu matumizi ya kiasi cha Sh. 665.3 Mil na chanzo cha fedha hizo kabla ya muda wa kazi kesho.
Ofisa huyo ametakiwa kuwasiliana na Ofisi ya Rais Utumishi ili kuhakikisha nafasi za kazi zinazokaimiwa zinajazwa mapema iwezekanavyo ili kuongeza ufanisi wa sekretalieti katika Mkoa wa Dodoma.
Agizo la saba lililotolewa na PAC kwa Mkoa wa Dodoma amesema, kwa kuwa hoja nyingi za ukaguzi bado hazijapata majibu sahihi, kamati kamati inatoa muda wa miezi sita kwa sekretarieti kukamilisho hoja za kukaguzi na taarifa ya utekelezaji ziwasilishwe kwa CAG na kwa kamati kabla ya miezi sita kuisha.

WHY Raila MUST be CORD Flag bearer to FACE OFF with Uhuru and VANQUISH Jubilee in 2017 General Election

To some he is Agwambo, to others, he is Owadgi Akinyi. To the Kalenjins he is Arap Mibei. To the Luhyas, he is Royalty from the lineage of Nabongo Mumia. To the Bukusu he is carries the Masinde Muliro torch of a free, just and liberated Kenyan-State. Behind him is a 38-40 tribe ethnic coalition support, compared to Uhuru’s 2.
Out of historical lessons learned, he has yearned for a united Kenya. He is effectively, the unofficial symbol of national unity. Whether its the Waiguru debacle or IEBC imbroglio, as Raila tongue enunciates, so does the nation pronounciate. Raila is the fulcrum of our national politics, the epicenter of our national consciousness, and the guarantor of our aspirations as a people.
Raila has the keys to unlocking our entrapment in a hole-country, which has refused to transform into a nation-state. Raila holds these truths as truly evident, that all Kenyans are created equal, all dwelling in “Unity, Peace and Liberty” as well described and inscribed in our national anthem.
Born in a household that was on a round the clock radar by the colonialists, and spied on round the clock by successive regimes, Rt. Hon. Raila Odinga, has been a victim of brutality by the powers that be, right from his childhood. And despite being in a position to sit pretty at the center of powers that be and amass himself wealth, status and comfort, Raila has dedicated his lifelong career to delivering the poor Kenyan masses from obscurity, mediocrity and poverty.
As a nation where successive regimes have sought to impose their dictatorial tendencies on the people, Raila has since the 80s under the shadow of Jaramogi, and later in the 90s, as his own man been the firewall that successive regimes have found tough to crack.
As the man standing in the way of their devious and mischievous ways, they have unsuccessfully dedicated entire state machinery towards maiming and taming him. He has won twice, his election stolen, but each time has humbled himself and agreed to serve the nation under any capacity. After all those who don’t agree to be led, cannot lead.
I have read, watched and understood this man to be an incredible man worth entrusting the reins of leadership of this country. All of us understand that Raila is the only one among-st the cast seeking CORD’s ticket, who knows what to do with the power when and if he gets it in August 2017.
Raila understands that this nation needs to be pushed out of the precipice of mediocrity and poverty. He has in numerous speeches highlighted why Kenya needs to catch up with the Singapore, Malaysia, and South Korea, nations which were at economic par with Kenya in the 60s. And at the foundation of stimulating unprecedented and sustained 10-12% annual growth is freedom.
Raila, as a victim of state emasculation and detention in the 90s, understands that individual freedoms mean free markets revolution, and growth, where individuals are allowed and given the incentives and resources to imagine, and explore those imaginations.
I don’t know what the other CORD principals would do, but Raila’s first 100 days’ agenda would be a period of massive overhaul of the Kenyan nation-state foundations, and reorientation of our nationalism with the ideals upon which the founders fought for independence.
Whether its Obama, Theresa May, Mandela, the measure of a leader is always going to be how much they understand the very articles of establishment of their nation at its founding, what they know about how the nation has deviated from those articles, and ultimately what their agenda is within 100 days to reorient the nation towards those ideals, and then institute an effective quality control and assurance mechanism to ascertain that his officers are on the same page in reclaiming Kenya’s lost glory and put Kenya on the path of sustained, unmatched and unprecedented economic growth, that will put our jobless youth to work.
I have listened to the entire crowd of presidential wannabees, and there’s not one who can look you in the eye, and tell you that they will rid this nation of cartels that threaten the very fabric of Kenya. And more importantly, none of them have the guts, and tried and tested history of unseating a sitting president. Raila led the struggle to defeat Kibaki in the 2005 referendum and then the subsequent 2007 election. And to date continues to be the shoulder upon which -the downtrodden and emasculated masses who are victims of Jubilee mismanaged, corrupt and inept economy- can lean on.
At a time when this country needs strong leadership devoid of corruption, Raila is the only man with the balls to guarantee that this nation is rid of all corruption cartels, that taxes aren’t evaded by the rich, that the Nairobi Stock exchange isn’t a hall for cleansing Eurobond/corruption money, and that all monies, stolen from Eurobond, NYS and stashed offshore are recouped back into the national coffers and reinvested into redeeming the youth from perpetual impoverishment and hostage by the corrupt and inept Kenyan regime.
In 2017, a Kenyatta is the incumbent, and only a political head to head matchup of Kenyatta vs Odinga, can excite the left wing bases of this country. It’s all about history.
The other is predictability. Having won every nationwide political contest since 2002, winning the 2005 referendum, 2007&2013 presidential elections, Raila is the only leader with a known voting pattern.
Looking at the 2013 math, its obvious that so long as he sweeps the Western voting block of Nyanza and Western, and guards against rigging, then retains the same voting pattern of his 38 to 40 tribes voting block, then he will easily romp home to victory by noon on voting day. The rest of the cast Kalonzo, Wetangula and Mudavadi haven’t delivered a national electoral voting map of Raila’s scale and magnitude, yet the stakes are so high for CORD to lose the 2017 election. Raila is the only man with a sure and tested path to victory in 2017. Anyone else is “kubahatisha”. NSIS will sponsor a ton of polling data to divert CORD from the trophy Raila presidency
As the eldest in the group, he is the only man who guarantees unity in the opposition. All the CORD presidential wannabees want a Raila endorsement, and campaign financing. And so if he endorses Wetangula for example, Kalonzo feels bad, if he picks Wetangula, and Wetangula would use that as an excuse to join Jubilee. If he picks Mudavadi, Kalonzo and Wetangula will claim Mudavadi is a Johnie-come-lately choking up their “patrimonial birthright”. And so a Raila candidature will unite CORD, as the other candidates would be disruptive, with the end result unknown.
Raila’s age also guarantees a succession plan, which is a major problem in Jubilee, where Ruto claims he is the only one entitled to succeed Uhuru yet we know Uhuru is intent on a third and fourth term, through removal of term limits. Raila can run to correct the wrongs in one term, then hand the leadership baton to Kalonzo, Weta or MaDvD. Raila can promise a one term presidency, but in their 50s and 60s, Kalonzo, Weta, or Mudavadi cannot promise the other, because they will want 2 terms.
Raila was PM for 5 yrs, executed some reforms which are anchored in the constitution, like the bill of Rights, which was Raila’s irreducible minimum. He wanted parliamentary system, but so long as the Bill of Rights wasn’t tampered with, he was willing to compromise, which is how our Bill of Rights is one of the most progressive in the world.
Raila is keen on operationalizing the freedoms as enshrined in the 2010 constitution, but which Jubilee has relegated to the back burner. Raila has a very concrete agenda as to what he needs as he finalizes a few aspects of a new republic that will be born in August 2017.
Maybe Kalonzo, Weta or Mudavadi may win in 2017, but that’s a gamble. The surest way for CORD to win would be the inevitable and incredible candidature of Raila Amolo Odinga. He has ran 3 times, won twice, and lost once. He can rule for 5yrs, and hand over the baton to Kalonzo, Joho, Weta or Mudavadi in 2022.

Hon Jim Bonnie: My Take on Raila Mudavadi RE-UNION!

It is reported that the son of Mudamba is in “secret” talks with ODM numero uno, Hon Raila Odinga, for a possible deal.
Mudavadi himself has given strongest indications that he might work with Odinga in a pre-election pact that is yet to be penciled in.
This however isn’t news for keen political observes. Odinga has nothing to reap from this reunion but it’s necessary nonetheless.
Suffice it to say, the biggest winner in this case would be Mudavadi. He’ll get any swat he chooses to go for but presidency.
My crystal ball tells me the man from Vihiga might vie for governorship. Though I don’t have the balls to tell which County he’ll settle for.
With Mr. Odinga’s blessings, Mudavadi might win as he prepare for a serious stab at presidency in 2022 without jokers like Kioni.
However, Raila’s candidature needs the full backing of Kalonzo Musyoka, the “man of God” From Tseikuru.
If Kalonzo backs him again, then Jakom might show a good performance in the upcoming elections (I’m not talking about a win).
But if Kalonzo insists on running for presidency, then he will cart away over one million Kamba votes Raila scooped in 2017.
This will nip Mr Odinga’s presidential bid in the bud and those who want to commit suicide for this reason will have a good excuse.

Habari Nzito: SPIKA WA BUNGE LA TZ JOB NDUGAI KIBOKO AFUNGUKA MAZITO KILA MMOJA ASIFIA KWA UAMUZI WAKE

Akijibu Maswali yamoja kwa moja ya Mwandishi wa habari, Spika wa Tanzania Job Ndugai, amesema anasikitishwa na Wabunge wa UKAWA na Tabia yao ya kutoka Nje. Japo ni haki yao kutoka nje lakini hivi karibuni imezidi. Japo itaendelea hivi tutakuwa hatujengi nchi amesema.

Ameahidi yeye mwenyekiti wa Bunge na naibu Spika watakaa na UKAWA wamalize hili tatizo kwani haipendezi spika unakaa mtu anatoka nje.

Amesema Sasa Nchi hii Migogoro, utengano umezidi, ni jukumu letu kama Viongozi kumaliza hii hali.

Kasema Wabunge waliofungiwa ilitokana na matomeo ya sintofahamu. Kwani kabla ya kufungiwa tunaomba Mbunge afute kauli yake, arekebishe au alete ushahidi. Pale anapokaidi huitwa kutoa ushahidi lakini saa nyingine hukataa. Mfano kuna Mbunge alisema polisi wameleta Magari ya Washawasha 700. Tulipomwambia alete ushahidi akasema alisoma Kwenye JamiiForums. Kama bunge hatuwezi fanya kazi kwa kutengemea Mitandao

Anasema hii hali inayoendelea bungeni inachochea chuki na Migogoro. Ni bora sasa tukaa nchini kama taifa ili tumalize hii hali.

Anasema kama Spika hatavumilia vijembe na kejeli kuendelea Bungeni
Ni haki ya mbunge kutoka nje. Lakini wale waliobaki nao wanawashambulia waliotoka, hili nalo ni tatizo. Wabunge wakitoka nje mambo mengi huharibika. Inachafua hali ya hewa. Uchaguzi unapoisha, siasa huhamia Bungeni.

Tunachukulia Mbunge kama mtu mzima. Chama tawala na UKAWA na sisi tukae chini tuongelee hili swala.

Wabunge wamezoea kuona Spika na Naibu wake wakiwa wabunge wa kuchaguliwa, hii ya naibu Spika kuwa wa kuteuliwa wanahofu kwamba atakuwa anapokea maelekezo kutoka Sehemu Fulani. Naomba niwahakikishie kwamba, sisi hatupokei maelekezo kutoka sehemu yoyote bali tunatoa maamuzi yetu tunavyoona inafaa. Hivo watuamini.
Older Posts
© Copyright CHUNGU CHETU | Designed By CHUNGU CHETU
Back To Top